0



Timu ya taifa ya Ivory Coast imetwaa kombe la mataifa ya Africa baada ya kuifunga Ghana  kwa penalt i9-8 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo ulifanyika katika uwanja wa Bata, Equatorial Guinea.




Historia imejirudia kwa Tembo kuwafunga Black Stars kwa penalti katiak fainali kama ilivyokuwa mwaka 1992 walipotwaa taji lao la kwanza.
Shujaa wa Ivory Coast leo aliuwa kipa wao Boubakar Barry aliefunga penalti ya mwisho akitoka kuokoa mkwaju wa kipa mwenzake Razak Braimah na kumaliza kiu ya miaka 23 ya kutotwaa ubingwa wa taji hilo.

Penalti za Ivory Coast zilifungwa na Aurier, Doumbia, Yaya Toure, Solomon Kalou, Kole Toure, Kanon Bailly Sery Die na Barry wakati Wilfred Bonny na Tallo walikosa. kwa upande wa Ghana waliofunga ni Mubarak Wakaso, Joedan Ayew,Adrew Ayew, Mensah Agyeima Badu Affial baba na Brimah walikosa,
Rais wa Equatorial Guinea Teodoro Obiang  na Rais wa FIFA Sepp Blatter awali walikuwepo uwanjani kukagua vikosi na baadaye kugawa medali na   kombe kwa mshindi.






Post a Comment

 
Top